Watu milioni moja sasa wamefungasha virago na kuukimbia mji wa Rafah kusini mwa Gaza, ka mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, huku kukiwa na ripoti mpya za mashambulizi ya usiku kuamkia leo katika maeneo ya kusini, kati na kaskazini yanayofanywa na vikosi vya Israel. Katika tarifa yake iliyotolewa leo kupitia mtandao wa kijamii wa X UNRWA imesema mji wa Rafah kwenye mpaka wa kusini wa Gaza na Misri ulikuwa nyumbani kwa zaidi ya watu milioni moja waliokimbia makazi yao kwa karibu miezi minane ya mashambulizi ya kila siku ya jeshi la Israel, kujibu shambulio la kigaidi lililoongozwa na Hamas kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba mwaka jana."Maelfu ya familia sasa wanaishi katika vituo vilivyoharibiwa na kusambaratishwa huko Khan Younis ambapo UNRWA inaendelea kutoa huduma muhimu, licha ya changamoto zinazoongezeka. Masharti hayaelezeki,” Haya yanajiri siku tatu tangu Rais wa Marekani Joe Biden kuzindua pendekezo la usitishaji mapigano kwa kuzingatia usitishaji wa hatua kwa hatua kwa vita hiyo, pendekezo likiripotiwa kujumuisha kuondolewa kwa majeshi ya Israel kutoka maeneo wyalikorundikana, kuachiliwa kwa mateka wa Israel na wafungwa wa Kipalestina, pamoja na mpango wa ujenzi mpya wa Gaza.Kulingana na UNRWA, maelfu ya familia zimelazimika kutafuta makazi katika majengo yaliyoharibiwa vibaya huko Khan Younis jiji ambalo liko kaskazini mwa Rafah, na linakadiriwa kuwa na watu wapatao milioni 1.7. Imeripotiwa kwamba makao yote 36 ya UNRWA huko Rafah sasa yamesalia matupu.Shirika hilo limeongeza kuwa Takriban wanawake na wasichana 690,000 wanaaminika kukosa vifaa vya msingi vya usafi wakati wa hedhi, faragha na maji ya kunywa.Ikiangazia mapambano ya kila siku yanayowakabili watu walio hatarini sana huko Gaza, UNRWA imelinukuu Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya uzazi UNFPA ambalo linakadiria kwamba karibu wanawake 18,500 wajawazito wamelazimika kukimbia Rafah. "Takriban 10,000 zaidi wamesalia huko katika hali mbaya na upatikanaji wa huduma za afya na vifaa vya uzazi ni mdogo. Afya ya mama na mtoto iko hatarini.”Likirejea wasiwasi huo mkubwa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP kupitia Matthew Hollingworth, Mkurugenzi wa WFP katika eneo linalokaliwa la Palestina lisema sasa hakuna "kikubwa tunachoweza kuwafanyia watu ambao bado wako Rafah, ambako barabara si salama, hazifikiki vizuri, na washirika wetu wengi na mashirika mengine ya kibinadamu yametawanywa”.Ameonya kwamba hofu ya afya ya umma sasa imevuka viwango vya janga, wakati sauti, harufu, na maisha ya kila siku, ni ya kutisha na ya kuzimu. Watu "wamekimbilia maeneo ambayo maji safi, vifaa vya matibabu na usaidizi havitoshi, usambazaji wa chakula ni mdogo, na mawasiliano ya simu yamesitishwa."